The Standard Group Plc is a
multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper
print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key
influence in matters of national and international interest.
Wizara ya Ardhi imezishtumu serikali za Kaunti na Makundi ya kidini kwa kuhujumu juhudi zake za kuzitwaa ardhi za shule, hospitali na misitu zilizonyakuliwa.
Kulingana na Waziri Jacob Kaimenyi serikali nyingi za kaunti hazijafahamu kuwa hati miliki zilizokuwa zimekabidhiwa serikali za wilaya sasa zipo chini ya hazina kuu ya kitaifa.
Aidha waziri ameyashtumu makundi ya kidini kwa kukataa kutoa hatimiliki za shule za umma walizokuwa wakiziongoza na sasa hivi ziko chini ya serikali.
Kaimenyi ameongeza serikali inafanya kila juhudi kuhakikisha inazitwaa ardhi zilionyakuliwa na watu binafsi huku akidokeza kuwa sababu kuu ya ardhi za shule za umma kunyakuliwa ni kwa sababu zipo katika sehemu zenye uvutio mkubwa.
Wakati uo huo amesema kuwa kwa ushirikiano na Tume ya Kitaifa ya Ardhi na Wizara ya Afya wanazikagua ardhi za hospitali zote nchini ili kuhakikisha zinapata hati miliki.
Premium Article
Get Full Access for Ksh299/Week.
Fact-first reporting that puts you at the heart of the newsroom. Subscribe for full access.
🔥 Flash Sale !
Subscribe now and enjoy 50% off monthly and annual plans. Offer ends in…
Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.
Journalism can't be free because the truth demands investment.
At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate,
factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the
pursuit of credible journalism.