Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Home To Bold Columnists
★★★★ - on Play Store
Download App

Utendakazi wa Jopo la Kumchunguza Jaji Tunoi Wafikia Kikomo

Jopo lililokuwa likichunguza madai ya ufisadi dhidi ya aliyekuwa Jaji wa Mahakama ya Juu Philip Tunoi litalazimika kuwasilisha ripoti yake ya uchunguzi bila mapendekezo kuhusu uchunguzi uliofanywa dhidi yake.
Mwenyekiti wa jopo hilo, Sharad Rao amesema hali hiyo imetokana na uamuzi wa Mahakama ya Juu iliyodumisha uamuzi wa Mahakama ya Rufaa wa kustaafu kwa majaji wakiwa na umri wa miaka sabini. Jopo hilo lina mamlaka ya kumchunguza jaji anayehudumu pekee. Kustaafishwa kwa Jaji Tunoi baada ya kufikisha umri wa miaka sabini na miwili kunamaanisha kwamba jopo lililokuwa likimchunguza halitaendelea tena na vikao hivyo.   
Kupitia wakili wake Fred Ngatia, Tunoi amekubali uamuzi wa kusitishwa kwa vikao hivyo. Awali, alitaka jopo hilo liendeleze vikao vyenyewe hadi tamati ili kumwondolea tope la kuhusishwa na tuhuma za kupokea hongo.
Mlalamishi Geoffrey Kiplagat alidai kuwa Tunoi alipokea hongo ya shilingi milioni 200 kutoka kwa Gavana wa Nairobi Evans Kidero ili kushawishi uamuzi kwenye kesi iliyopinga kuchaguliwa kwa Kidero kuwa Gavana wa Nairobi.

Na, Beatrice Maganga

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Uncover the stories others won't tell. Subscribe now for exclusive access.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902

Related Topics

philip tunoi