''Hatujamuidhinisha Wetangula'' wasema wajumbe wa Ford Kenya

Na Carren Omae

Mvutano unatishia kuzuka katika Chama cha Ford Kenya baada ya baadhi ya wajumbe kukana madai ya kumwidhinisha kiongozi wao ambaye pia ni mmoja wa vinara wa CORD, Moses Wetangula kuwania urais wakati wa uchaguzi mkuu ujao. Wakati wa kikao na wanahabari jijini Kisumu, wajumbe hao kutoka maeneo mbalimbali nchini wamempa Wetangula makataa ya siku kumi na nne kuandaa Kongamano la Kitaifa na Wajumbe kuwachagua viongozi wa chama, vilevile atakayewania urais. Ken Wafula ni Mwenyekiti wa Muda wa chama hicho.

Aidha amemshtumu kwa madai ya usimamizi mbaya wa chama huku akisema anayabagua baadhi ya maeneo huku akizingatia eneo la Magharibi pekee.
Wajumbe hao wamepinga uteuzi wa Seneta wa Kakamega, Bonny Khalwale kuwa Naibu Kiongozi wa chama wakisema uteuzi wake haukufanywa kwa njia inayofaa.