Wanafunzi wahakikishiwa kupewa mikopo ya HELB

Na, Mike Nyagwoka

Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu HELB imewahakikishia wanafunzi wote wanaojiunga na vyuo vikuu mwezi huu na mwezi ujao kuwa watapata mikopo hiyo ila itachelewa. Kwa mujibu wa Afisa Mkuu Mtendaji wa bodi hiyo, Charles Ringera, HELB imeomba orodha ya wanafunzi wote wanaotarajia kujiunga na vyuo ili fedha za mikopo zitayarishwe mapema.
Haya yanajiri huku bodi hiyo ikiongeza kiwango cha mikopo inayotolewa kwa wanafunzi, hadi shilingi elfu 40 kutoka shilingi elfu 35 kwa wanaopata kiwango cha chini zaidi. Aidha mkopo wa juu zaidi utawa shilingi elfu 60 kutoka shilingi elfu 50. Afisa Mkuu Mtendaji wa HELB, Charles Ringera amesema hatua hii imechukuliwa ili kuwalinda wanafunzi kutokana na kupanda kwa gharama ya maisha.
 

 

Related Topics