Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Join Thousands Daily
★★★★ - on Play Store
Download App

Serikali yatoa marufuku ya kutotoka nje Mandera

Na Carren Omae na Frederick Muitiriri

Kufuatia shambulio katika Kaunti ya Mandera siku ya Jumanne ambapo jumla ya watu kumi na wawili waliuliwa, serikali imetangaza Marufuku ya kutotoka nje eneo hilo. Waziri wa Masula ya Ndani ya Nchi, Joseph Nkaiserry amesema wakazi hawatatakIwa kutoka nje kuanzia saa kumi na mbili unusu jioni hadi saa kumi na mbili unusu asubuhi katika kipindi cha miezi miwili kuanzia leo hii hadi Disemba 27.
Maeneo yatakayoathirika na marufuku hayo ni Mandera Mjini, Omar Jillo, Arabia, Fino, Lafey Kotulo, Elwak na maeneo yaliyo umbali wa kilomita ishirini kutoka mpaka wa Kenya na Somalia.
Wakati uo huo, Mahakama ya Mandera imewaruhusu maafisa wa polisi wa kitengo cha kukabili ugaidi, ATPU kumzulia mlinzi Abdirahman Ali wa Hoteli ya Baasharo kwa siku kumi. Kulingana na maafisa wa polisi, Abdirahman Ali mwenye umri wa miaka ishirini na mmoja anashukiwa kuwasaidia magaidi hao kutekeleza shambulio hilo. Inadaiwa kwamba hakulala katika hoteli hiyo usiku wa shambulio ilivyo kawaida. Inasemekana kwamba usiku huo, alilala katika jengo tofauti lililo umbali wa mita 15 kutoka hoteli hiyo. Aidha anashtumiwa kwa kutoripoti kisa hicho suala ambalo amelipinga.
Mahakama imekubali ombi la maafisa wa polisi ikisema uchunguzi zaidi lazima ufanywe ili kuzuia mashambulio zaidi. Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 7 mwezi ujao.

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Bold Reporting Takes Time, Courage and Investment. Stand With Us.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902