Ruto dismisses charges - Swahili

Mbunge wa Eldoret kaskazini William Ruto sasa amejitokeza waziwazi na kusema kuwa mashtaka alio nayo Luis Moreno Ocampo kumhusu hayana ukweli wowote. Ruto amedokeza kuwa Ocampo anatumia uvumi mtupu kumhusu ambao haupaswi kuchukuliwa kwa uzito wowote , William Ruto ni kiongozi wa kwanza kujitokeza kuzungumzia mashtaka ya Ocampo siku mbili baada ya mawakili wa William Ruto, Henry Kosgei na Joshua Sang kukabidhiwa rasmi mashataka yanayowakabili wateja wao. Kesi za watatu hao zinatarajiwa kusikilizwa tarehe 1 mwezi ujao katika mahakama ya ICC jijini the Hague Uholanzi.