Mbwa Wapewa Chanjo Mombasa

Madktari wa wanyama  wamekita kambi  katika eneo  la   kinango  huko pwani ili  kutoa chanjo za bure kwa mbwa na paka katika sehemu hiyo. Zoezi hilo linaloendelea  linalenga mbwa elfu hamsini katikasehemu hiyo ili kuzuia
kuambukizw kwa ugonjwa  hatari wa kichaa cha mbwa ambao unambukizwa  kutoka kwa wanyama   hasa   mbwa   hadi kwa binadamu. Ugonjwa huo hauna tiba.