Athari na hatari za pombe haramu ya chang’aa iliyonywewa mtaani Kibera- laini saba mwishoni mwa wiki zingali hadi sasa zinadhihirika miongozi mwa waliokunywa kileo hicho hatari. Frank Otieno anaendelea kufuatilia na hii leo amebaini kwamba watu wangali wanaaga dunuia, wengine wakipofuka na kukosa uwezo wa kuona ilhali wengine wanasemekana kuumia mafichoni na huenda idadi ya walioaga ambayo imekwea hadi watu 23 hii leo ikaongezeka hata zaidi.