Washukiwa Wa Uchochezi

Naibu wa waziri wa barabara Wilfred Machage, wabunge Fred Kapondi na Joshua Kutuny walikamatwa hii leo na kufikishwa katika makao makuu ya  upelelezi ya CID hapa jijini  kwa  mahojiano na polisi kuhusu matamshi ya uchochezi. Washukiwa hao  wangali wanazuiliwa na polisi huku kamishina wa polisi Mathew Iteere akitangaza mapema leo kwamba watafikishwa mahakamani wakati wowote.