Naibu wa waziri wa barabara Wilfred Machage, wabunge Fred Kapondi na Joshua Kutuny walikamatwa hii leo na kufikishwa katika makao makuu ya upelelezi ya CID hapa jijini kwa mahojiano na polisi kuhusu matamshi ya uchochezi. Washukiwa hao wangali wanazuiliwa na polisi huku kamishina wa polisi Mathew Iteere akitangaza mapema leo kwamba watafikishwa mahakamani wakati wowote.