The Standard Group Plc is a
multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper
print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key
influence in matters of national and international interest.
Wakenya wote walio
na vitambulisho vya zamani wataruhusiwa kujiandikisha kama
wapiga-kura ili kushiriki katika kura ya rasimu ya katiba inayotarajiwa hivi
karibuni. Uamuzi huu umetangazwa na waziri wa uhamiaji Otieno Kajwang baada ya
kutumiwa maombi na tume ya muda ya uchaguzi IIEC. Kajwang’ hata hivyo alisema
walio na vitambulisho vya zamani hawataruhusiwa kujisajili kushirikia katika
uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2012. Wakati huo huo zoezi la kuwasajili wapiga kura
kwenye eneo bunge la mvita lilitibuliwa na maafisa wa polisi pale mwanawe
aliyekuwa mbunge wa eneo hilo, Abduswamad Shariff Nassir alipojaribu kuongoza
zoezi hilo, huku maafisa wa polisi wakitaja mkusanyiko huo kama usio halali na
kuwatawanya kwa kutumia vitoa machozi.