Pirates kidnap Kenyan sailors

Mabaharia 17 miongoni mwao wakenya 10 ni miongoni mwa waliotekwa nyara na maharamia wa kisomali katika bahari hindi wakiwa katika shughuli ya uvuvi. Hii ni baada ya maharamia hao kuiteka nyara meli ya mabaharia hao inayomilikiwa na kampuni moja ya uhispania. Wamiliki wa meli hiyo wameripotiwa kuwa safarini kuelekea Mombasa kuanzisha mazungumzo yatakayopelekea kuachiliwa kwa meli hiyo. Hata hivyo maharamia walioiteka nyara meli hiyo hawajawasiliana na wamiliki wake kuwafahamisha iwapo watahitaji fedha kiasi kipi ili kuiachilia meli.