Raila Kibaki on tracking funds

Serikali itawasilisha bungeni hivi karibuni mswada wa kuwezesha serikali kuwafuata washukiwa wa ufisadi hata wakihamia nchi nyingine.Waziri mkuu Raila Odinga amesema leo kwenye kongamano la euromoney hapa jijini kwamba serikali imependekeza mswada huo ambao utajulikana kama mutual legal assistance bill. Aidha Raila alisema serikali itafanya juhudi kuwapa wakenya wenye mapato madogo kwenye miji chakula kwa bei nafuu lakini hakusema ni lini mradi huo utaanza. Kongamano hilo lilifunguliwa na rais Mwai Kibaki na unaisha kesho.