×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]

Bilionea wa uturuki azuiliwa kwa madai ya kufadhili ugaidi

News
  Bilionea wa Uturuki Elsek Osman na mwenzake Gokmen Sandikci. [Robert Menza, Standard]

Mahakama mjini Mombasa imeamuru bilionea wa Uturuki Elsek Osman na mwenzake Gokmen Sandikci kuzuiliwa kwa siku kumi na nne huku uchunguzi ukiendelea kuhusu madai ya kufadhili ugaidi yanayowakabili.

Hakimu Mkazi David Odhiambo amesema kuwa kesi inayowakabili wawili hao ni nyeti kwa sababu inahusu usalama wa taifa.

Ameongeza kuwa serikali imewasilisha ushahidi mzito chini ya Sheria ya Kuzuia Ugaidi, POTA.

Hakimu Odhiambo pia ameagiza kuwa washukiwa hao wapewe huduma ya matibabu endapo watahitaji, pamoja na kuruhusiwa kuwasiliana na mawakili wao kabla ya kurejeshwa mahakamani tarehe ishirini na saba mwezi huu wa Januari.

Elsek Osman, ambaye ni mkimbizi wa Uturuki, alikamatwa Januari kumi na tatu katika eneo la Mtwapa, Kaunti ya Kilifi, kufuatia kisa cha ghasia za barabarani kilichohusisha gari lake aina ya V8 na msafara uliokuwa ukimsafirisha Gavana wa Wajir pamoja na Afisa Mwandamizi wa Kaunti ya Kilifi.

Mawakili wa Osman, wakiongozwa na John Khaminwa na Cliff Ombeta, wamesema kuwa mteja wao anatuhumiwa kwa madai mazito ya kufadhili ugaidi ilhali ni mkimbizi ambaye amekuwa akiishi nchini Kenya kwa zaidi ya miaka ishirini.

Wakili Khaminwa ameiambia mahakama kuwa Osman ana uwekezaji unaokadiriwa kufikia shilingi bilioni sita nchini Kenya na pia anafadhili zaidi ya wanafunzi mia tatu kwa kuwalipia karo.

Imeelezwa kuwa Osman aliingia nchini kama mkimbizi baada ya kutofautiana na Serikali ya Uturuki, hali iliyomlazimu kutafuta hifadhi nchini Kenya.

Related Topics


.

Similar Articles

.

Latest Articles

.

Recommended Articles