×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]

Cyrus Jirongo afariki baada ya ajali barabarani

News

 

 Aliyekuwa Waziri na Mbunge wa zamani wa Lugari, Cyrus Jirongo, amefariki dunia kufuatia ajali ya barabarani eneo la Karai.

Aliyekuwa Waziri na Mbunge wa zamani wa Lugari, Cyrus Jirongo, amefariki dunia kufuatia ajali ya barabarani eneo la Karai, Naivasha, kwenye barabara kuu ya Nairobi–Nakuru.

Kwa mujibu wa maafisa wa polisi, ajali hiyo ilitokea majira ya saa tisa asubuhi, wakati Jirongo alipokuwa akiendesha gari lake kutoka Nakuru kuelekea Nairobi.

Gari lake liligongana ana kwa ana na basi lililokuwa likitokea upande wa pili wa barabara, na kusababisha kifo chake papo hapo.

Taarifa ya kifo chake imethibitishwa na DCIO wa Naivasha, Isaac Kiama, aliyesema kuwa uchunguzi wa awali unaashiria kuwa ajali hiyo ilitokana na mgongano wa moja kwa moja kati ya magari hayo mawili.

Kifo cha Jirongo kimepokelewa kwa mshtuko mkubwa kutoka kwa viongozi wa kisiasa, jamaa, marafiki na wananchi kwa ujumla, wengi wakimtaja kama kiongozi mwenye ushawishi mkubwa aliyewahi kuwa na nafasi muhimu katika siasa za nchi.

Katika maisha yake ya kisiasa, Jirongo aliwahi kuhudumu kama Waziri na pia Mbunge wa Lugari, akijijengea jina kama mwanasiasa jasiri, mwenye kauli kali na msimamo thabiti. Alijulikana pia kwa mchango wake katika siasa za chama tawala cha wakati huo na ushawishi wake mkubwa hasa miongoni mwa vijana.

Urithi wake unaacha taswira ya maisha yaliyojaa mafanikio, changamoto na utata, huku taifa likiendelea kuomboleza kifo cha mmoja wa watu waliowahi kuwa na athari kubwa katika uwanja wa siasa za Kenya.

Related Topics


.

Similar Articles

.

Latest Articles

.

Recommended Articles