×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]

Krismasi sio kula tu

News
 Kristmasi sio kula tu [Picha: Hisani]

Jameni tumeingia msimu wa sikukuu tupende tusipende , na msimu huu huja na mwembwe na mahanjam yake sio haba.

Ni wakati huu ndio utapata watu wakiwa na tabia za kushangaza mno , tabia ambazo hujitokeza tuu msimu huu.Sijui kama ni pupa , au ni msisimko wa kupindukia bali tabia za kina yakhe wengine huwa za udhi kweli!

Kila siku ya maisha inapaswa isherehekewe mradi uko hai , unapumua , na unauzima wa mwili basi kila siku unasababu ya kuwa na furaha usijeukawa unasiku za furaha na zile zenye karaha .

Linalo udhi mno wakati kama huu ni jinsi watu wengine hula , yaani utawapa watu wakila chakula kana kwamba msimu wa sikukuu huwa wameongezwa tumbo la pili , mtu kama yule anakula chakula kiingi hadi inamshinda kutembea au cha mno anaanza kuugua kwa kula saana , sikukuu kama hii haimaniishi ukala saana kama kawaida.

Wengine pia unawapata wanakunywa pombe kupindukia yaani kwa siku tano hivi mfululizo atakuwa anabugia pombe bila kujali eti ni sikukuu , hapana.

Hebu tuwe n mtazamo mpya wa maana makhsusi wa sikukuu , mwanzo tukielewa fika kuwa sikukuu hii ilitengwa kihistoria kama siku ambayo yesu kristo alizaliwa basi uhusiano huo wakuzaliwa kwako na kula , kunywa kana kwamba dunia inakwisha uko wapi jameni ?

kwangu mie naamini kuwa sikukuu ambazo zinatukodolea macho zamaanisha wakati wa umoja wa jamii , ambao tunapaswa kudhihirisha upendo w kweli kwa kushirikiana pamoja . hebu tuwakumbuke ambao hawana cha kuita sikukuu msimu huu , hebu tukumbuke yatima , wafungwa magerezani , wagonjwa na watu masikini katika jamii , ndiposa tamaa yetu ya mwili ipungue

Tusijipende kupindukia , eti wakati kama huu umejinunulia nguo nyiingi na ndugu yako hana hata kiatu , eti wewe umechonga nywele na mamako kule kijijini anatembea uchi jameni tuweke tamaa nyuma na tuwatendee wengine mema.

Isiwe kuwa wewe umeenda holidei mombasa na watoto wako wako kijijini hohehahe.

Kwa kufanya hivyo tutakuwa tumeadhimisha kuzaliwa kwa yesu kristo ambaye kwa maisha yake tumemfahamu kama aliyejaa huruma na upendo , alikuwa mwingi wa rehema na msamaha , na pia tunapozungumza kuhusu msamaha hebu sasa tuwasamehe wote waliotukosea wakati huu tukuwe watu ambao wamejimwayamwaya kindanindani ili tusiwe na vikwazo mioyoni mwetu

Kutoka kwangu anne nawatakia sikukuu isiyokuwa na bugudha zoote wala walakin wanasema kwa kimombo merry chrismas!

wasIliana nami ; [email protected]

Related Topics


.

Popular this week

.

Latest Articles