National Super Alliance - NASA ndio muungano mkubwa zaidi wa upinzani kuwahi kuundwa nchini Kenya tangu uhuru ukijumuisha vyama vinne vikuu vya upinzani.
Muungano huo ulianzishwa muda mfupi kabla uchaguzi mkuu uliopita wa mwaka 2017 kama njia ya kuimarisha makabiliano na muungano wa Jubilee uliojumuisha vyama vya URP na TNA.