Aliyekuwa rais wa nchi ya Zimbabwe marehemu Robert Mugabe. [Picha: Standard]
Kifo cha Robert Mugabe baba wa taifa wa Zimbambwe na mdau mkongwe wa kisiasa Afrika kumezusha mjadala mkubwa miongoni mwa wasomi na wanafalsafa wa kimataifa kumuhusu. Je, Mugabe ametowa mchango gani barani Afrika na duniani kwa jumla? Je, alifaulu ama alishindwa katika azma yake ya ufanisi kwa aliowaongoza? Je, tunaweza kumuhukumu vipi bwana huyu tukitilia maanani mapungufu ya mwanadamu katika dunia ilosheheni changamoto sufufu za kisiasa, kiuchumi na kjamii? Mchanganuzi wa kisiasa pwani Abdulkadir Shtua asema Mugabe alianza vyema lakini mwisho akaharibu kutokana na kutakabari na kugeuka dikteta.