Lisemwalo lipo na kama halipo basi limo njiani laja ijapo kwa mwendo wa jongoo. Maisha ya kesho inamtegemea mtoto wa leo ambaye anayo miaka mitano hadi kumi (5-10) ambaye maadili yake itategemea jinsi atakavyolelewa na mzazi ama mwalimu wake.
Kuna Imani kubwa kwamba kuchaguliwa hivi majuzi kwa waziri wa elimu nchini, Professa George Albert Omore Magoha bila shaka kutalegeza kamba janga la shule kuwa mazizi ya anasa na ngono hususan katika kaunti ya Mombasa na Kenya nzima ambapo ni dhahiri wazi kwamba idara husika ama maafisa ambao wamekuwa na jukumu la kukomesha balaa hili wamefunikwa kwa nyuso za ufisadi baina yao na wenye kusimamia shule hizi.