Wakazi wa eneo la Kapsoit katika kaunti ya Kericho wamemsuta mwaniaji wa kiti cha urais katika muungano wa NASA Raila Odinga na kumtaja kuwa mwongo anapodai kuwa kilimo biashara katika eneo hilo sasa ni duni.
Katika matangazo ya moja kwa moja ya hutuba ya Bw Odinga eneo hilo, kupitia KTN News, wananchi waliskika wakisema kuwa eneo hilo ni ngome ya chama cha Jubilee.