Mwaka mpya wapiga hodi. Mwaka ambao wengi wana matajario ya mema na bora kutokea.Japokuwa huo ndio mtindo, makala haya yataangazia baadhi ya mambo ambayo hatufai kamwe kutarajia mwaka huu.
Naam, ni vyema kuwa na matarajio mwaka unapoanza kwa kuwa huwa inaongeza ari na hamaki ya kutia bidii lakini ni vyema kujua kwamba baadhi ya mambo hayataleta ufanisi maishani mwetu. Kwa kabisa tutambue kwamba kwenda kanisani na kusema kwamba baraka zako umezipokea kwa kuwa mchungaji amesema haitoshi.