Msako mkali unatarajiwa kuanzishwa asubuhi hii na maafisa wa Tume ya Huduma za Walimu, TSC dhidi ya walimu ambao hawajasajiliwa rasmi na tume hiyo lakini wanafunza katika shule za umma na za binafsi.
Msako huo unawalenga walimu ambao waliondolewa katika orodha ya TSC kwa sababu za nidhamu zikiwamo dhulma za ngono na wakarejea kufunza kwa kutumia njia za mkato.