Aliyekuwa Gavana wa Nairobi Evans Kidero akamatwa tena

Aliyekuwa Gavana wa Nairobi, Evans Kidero ametiwa mbaroni na maafisa wa EACC kufuatia tuhuma za hivi punde  zaidi za ufisadi.

 Kidero na liyekuwa Mkuu wa Wafanyakazi wa Kaunti ya Nairobi George Wainaina wametiwa mbaroni wakidaiwa kuilipa kampuni moja ya uwakili, shilingi milioni 68 kwa njia za ufisadi na utumizi mbaya wa mamlaka.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Mashtaka Noordin Hajj, Wawili hao walishirikiana na watu wengine 15 katika kufanikisha ulipaji wa fedha hizo kwa kampuni ya uwakili ya Wachira Mburu, Mwangi and Company Advocates.

 Wengine wanaolenga kufunguliwa mashtaka mbalimbali na waliokuwa maafisa wa  Kaunti ya Nairobi kadhalika iliyokuwa manispaa; Aduma Joshua, John Mwangi Kariuki na  Paul Mutunga Mutungi.

 Kadhalika maafisa kadhaa wa sasa kayika vitengo vya uhasibu na ukaguzi wanalengwa wakiwamo Manasseh Karanja,  Philomena Kavinya, Ng'ang'a Mungai, Charity Ndiritu, Pterson Andrew Njiru, Ekaya Alumasi, James Mimi Mbugua, Elizabeth Wanjiru Nderitu, Alice Njeri Mundia, Hannah Muthoni Kariuki na Mkurugenzi wa Kampuni ya Cups Limited John Ngari Wainaina.