Hatimaye Ivy Wangechi mwanafunzi wa chuo Kikuu cha Moi ambaye aliuliwa na aliyekuwa mpenziwe Naftali Kinuthia kwa kukatwa kwa shoka, amezikwa nyumbani kwao katika Kijiji cha Mahiga kwenye Kaunti ya Nyeri. Viongozi, jamaa na marafiki waliofika katika hafla ya mazishi wamekishtumu kitendo hicho cha mauaji huku wakimtaka mshukiwa afunguliwe mashtaka mara moja.
Ni siku ambayo imekuwa ya majonzi hasa baada ya Mwili wa Ivy Wangechi kuwasili katika uwanja wa Shule ya Msingi ya Mahiga.