Walanguzi wa mihadarati waonywa Mombasa

Kamanda wa Polisi Kaunti ya Mombasa Johnston Ipara amewaonya watu ambao wanaendeleza ulanguzi wa mihadarati kwenye maeneo ya jiji hilo kwamba watakabiliwa kwa mjibu wa sheria.

Amesisitiza kwamba idara ya Polisi inaendeleza msako wa kuwatia nguvuni walanguzi hao sawa na wale ambao wamekuwa wakitumiwa kusafirisha mihadarati ndani na nje ya Mombasa.

Hayo yanajiri huku washukiwa watatu wa ulanguzi wa dawa za kulevya wametiwa mbaroni katika visa vitatu tofauti.

Hayo yanajiri huku takwimu ya Mamlaka ya Kudhibiti Pombe na dawa za kulevya NACADA zikionesha kwamba jumla ya watu 24, 500 kwenye Kaunti ya Mombasa wameathiriwa na mihadarati.

Related Topics