Kamanda wa Polisi Kaunti ya Mombasa Johnston Ipara amewaonya watu ambao wanaendeleza ulanguzi wa mihadarati kwenye maeneo ya jiji hilo kwamba watakabiliwa kwa mjibu wa sheria.
Amesisitiza kwamba idara ya Polisi inaendeleza msako wa kuwatia nguvuni walanguzi hao sawa na wale ambao wamekuwa wakitumiwa kusafirisha mihadarati ndani na nje ya Mombasa.