Ziara ya Kalonzo maeneo ya kati inalenga kuwashawishi wakazi kumuunga mkono 2022

Kiongozi wa Chama cha Wiper Kalonzo Musyoka leo hii anatarajiwa kufanya ziara eneo la kati, huku akiaminika kwamba analenga kuwashawishi wakazi wa eneo hilo kumuunga mkono waati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2022.

Hii itakuwa mara ya sita kwa kipindi cha mwezi mmoja na nusu ambapo Kalonzo anafanya ziara eneo hilo. Kulingana na ratiba ni kwamba Kiongozi huyo wa Wiper anatarajiwa kuhudhuria ibada katika kanisa la Thika Township kwenye Kaunti ya Kiambu kabla ya kukutana na viongozi wa makanisha kisha kuendeleza ziara kwenye maeneo ya Meru na Embu.

Inaarifiwa ziara za Kalonzo kwenye kaunti za Kiambu, Nyeri na Muranga zinalenga kuwashawishi wapigakura kwamba ndiye anafaa kurithi kiti cha urais baada ya Rais Uhuru Kenyatta kustaafu mwaka 2022.

Related Topics