Maafisa wa polisi wamewanasa washukiwa tisa ambao wanahusishwa na misururu ya visa vya wizi wa kimabavu na ubakaji wa wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Maseno.
Mkurugenzi wa Idara ya Upelelezi DCI, George Kinoti amesema tisa hao wamenaswa baada ya kupashwa habari kutoka umma.
Kinoti amesema kwamba washukiwa hao wamenaswa na vifaa hatari vikiwamo panga na rungu. Aidha washukiwa wengi ambao walitoroka wakati wa opereshini hiyo, wanatafuatwa na polisi. Hatua hiyo ya polisi inafuatia lalama kutoka kwa wanafunzi wa chuo hicho, ambao wamekuwa wakiibiwa huku wanafunzi wa kike wakibakwa na watu wasiojulikana nyakati za usiku