Shule ya Wavulana ya upili ya Njoro kwenye Kaunti ya Nakuru imefungwa ghafla. Maafisa wa Elimu kwenye kaunti hiyo ya Nakuru walichukuwa hatua hiyo baada ya Mwalimu kugundua kuwa kulikuwa na petroli kwenye bweni moja ya shule hiyo inayotumiwa na zaidi ya Wanafunzi 70.
Haya yanajiri siku chache, baada ya bweni nyingine kuteketezwa na mali yenye dhamani isiyojulikana kuteketea. Wanafunzi wote walitumwa nyumbani baada ya maafisa wa Elimu, Usimamizi wa Shule na Maafisa wa usalama kufanya mkutano na kuafikia uamuzi huo.