Wawili wauliwa na mifugo kuiibwa kwenye Eneo la Kolowa mpakani pa kaunti za Baringo na Elgeyo Marakwet

Watu wawili wameuliwa huku idadi ya mifugo isiyojulikana ikiibwa na washukiwa wa wizi wa mifugo kwenye Eneo la Kolowa mpakani pa kaunti za Baringo na Elgeyo Marakwet.

Tukio hili limejiri siku chache tu baada ya mazishi ya watu watano wakiwamo polisi wa akiba kuzikwa baada ya kuuliwa kwa kupigwa risasi na washukiwa wa wizi wa mifugo kwenye kijiji cha Sogotei, Kaunti ya Baringo huku idadi isiyojulikana ya mifugo vilevile ikiibwa kwenye Eneo la Kolowa, Todoo Kaunti ya Elgeyo Marakwet.

Related Topics

cattle rustling