×
App Icon
The Standard e-Paper
Kenya’s Boldest Voice
★★★★ - on Play Store
Download App

Rais wa Sudan Omar Al Bashir aivunja serikali

Wasiwasi umetanda nchini Sudan baada ya Rais wa taifa hilo Omar Al Bashir kutangaza hali ya hatari na kuivunja serikali na kuwafuta kazi magava wote. Bashir alitoa tangazo hilo kupitia runinga za taifa hilo na kuwateua maafisa wa usalama kuchukua nafasi ya magavana hao. Katika siku za hivi karibuni maandamano yamekuwa yakiendelea nchini humo huku wanaopinga uongozi wake wakimtaka uondoka madarakani.

Hata hivyo katika taarifa yake, Bashir aliyataja maandamano hayo kuwa yanayolenga kutatiza ustawi wa nchi hivyo kutangaza hali ya hatari itakayodumu kwa kipindi cha mwaka mmoja. Vilevile alilitaka bunge la nchi hiyo kusitisha mabadiliko yoyote ya katiba ambayo yangeongeza muda wake wa kuhudumu.

Get Full Access for Ksh299/Week.
Fact‑first reporting that puts you at the heart of the newsroom. Subscribe for full access.
  • Unlimited access to all premium content
  • Uninterrupted ad-free browsing experience
  • Mobile-optimized reading experience
  • Weekly Newsletters
  • MPesa, Airtel Money and Cards accepted
Already a subscriber? Log in