Twalib Mbarak atarajiwa kuapishwa rasmi kuanza kuhudumu katika EACC

Afisa Mkuu Mtendaji wa Tume ya Maadili na Kukabili Ufisadi, EACC, Twalib Mbarak leo hii anatarajiwa kuapishwa rasmi kuanza majukumu yake katika tume hiyo. Jaji Mkuu, David Maraga ataongoza uapisho huo katika Mahakama ya Juu.

Kuapishwa kwake kunajiri baada ya Bunge la Kitaifa mwaka uliopita kuidhinisha uteuzi wake. Mbarak anachukua hatamu za uongozi kutoka kwa Halakhe Waqo ambaye muda wake wa kuhudumu ulikamilika.

Wakati alipohojiwa na Kamati ya Bunge ya Haki na Sheria kwa wadhifa huo, Mbarak aliahidi kutumia zaidi teknolojia kukabili ufisadi na kushikiriana na shirika la kutwaa mali ya umma iliyomilikiwa kinyume na sheria. Alisema atakuwa tayari kujiuzulu wadhifa wake kama litakuwapo shinikizo la kumtaka kuwa na mapendeleo katika utendakazi wake.

Related Topics

Mbarak EACC