Madaktari 100 kutoka Cuba wanatarajiwa kuwasili nchini tarehe 28 mwezi huu. Mkataba utakao waidhinisha madaktari hao nchini umetiwa saini na Baraza la Magavana na Wizara ya Afya.
Akizungumzia mkataba huo, Mkurugenzi wa Kamati ya Kaunti ya Tharaka Nithi, Dakta Gichuyia Nthuraku ametetea hatua hiyo akisema madaktari hao watakuwa tu wasaidizi wala hawaji kuchukua nafasi za madaktari wa humu nchini.