Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Stay Informed, Even Offline
★★★★ - on Play Store
Download App

Mkenya awasilisha sababu za kutaka kubanduka kwa makamishna wa IEBC

Huku kamati ya pamoja inayowajumuisha wabunge na maseneta wa Jubilee na CORD ikitarajiwa kuanza mazungumzo kuhusu hatima ya makamishna wa Tume ya Uchaguzi IEBC, kamati ya Haki na Sheria Bungeni imeanza vikao rasmi vya kusikiliza ombi lililowasilishwa na mkazi wa Bungoma, Barasa Kundu Nyukuri kuwataka makamishna wa tume hiyo kuondoka ofisini. Vikao hivyo vinaanza baada ya kamati hiyo pamoja na ile ya Bunge ya Utekelezaji Katiba, CIOC kupokea ombi hilo rasmi leo hii.
Kwenye vikao vya leo, Nyukuri ameelezea sababu za kuwasilisha ombi hilo. Akijibu maswali ya wabunge, mlalamishi huyo amesema ni kupitia bunge tu ndipo utaratibu wa kuwaondoa makamishna hao utatekelezwa, huku akielezea haja ya shughuli hiyo kuharakishwa ili kutoa nafasi kwa makamishna wengine kuteuliwa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.
Ameiambia kamati hiyo kwamba IEBC haiwezi kusimamia uchaguzi mkuu ujao, akidai kwamba imeshindwa kuwasajili wapiga-kura, mbali na kutilia shaka uhuru wa tume hiyo.

Na, Caren Omae

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Bold Reporting Takes Time, Courage and Investment. Stand With Us.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902

Follow The Standard on Google News

Related Topics

IEBC