Hata kabla ya 2017 kufika, wanasiasa wameanza kujipigia debe na kujitapa hadharani pasi na kutimiza ahadi zao kwa wapiga kura. Joto la kisiasa linalotanda nchini inasambaratisha maendeleo na utendakazi hivyo basi Wakenya watazidi kubakia katika lindi la umaskini. Ubishi kati ya Seneti na Bunge ni dhihirisho tosha kuwa viongozi tuliowachagua wana ubinafsi.
Wabunge wamekuwa joka la mdimu kwa kuzima juhudi za maseneta kujipatia fedha ili kuimarisha jukumu lao la uangalizi wa utendakazi wa serikali za kaunti, Aidha,ukweli wa methali kila mwamba ngozi huvutia kwake umedhihirika kwa sababu wamejitengea bilioni 35 za Hazina ya Maendeleo ya Maeneobunge (CDF) hata baada ya marufuku ya hazina hiyo kutangazwa na mahakama.