Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Join Thousands Daily
★★★★ - on Play Store
Download App

''Tutatoa msimamo wetu kuhusu waziri wa ugatuzi'' Lasema baraza la mashirika yasiyo ya serikali

Na Carren Omae

Baraza la Mungano wa Mashirika yasiyo ya Serikali mapema leo linatarajiwa kutoa taarifa kuhusu madai kwamba baadhi ya mashirika yalimhusisha Waziri wa Ugatuzi na Mipango ya Kitaifa Mwangi Kiunjuri katika sakata ya ufisadi. Mwenyekiti wa Mashirika hayo Stephene Cheboi amesema watatoa msimamo  kuhusu Waziri huyo.
Siku ya Jumatano Waziri Kiunjuri aliibandua Bodi ya Mashirika Yasiyo ya Serikali ikiwa siku moja tu baada ya bodi hiyo kumtuhumu kuwa aliitisha hongo baadhi ya mashirika hayo.
Hata hivyo mashirika hayo tayari yamejitenga na hati-kiapo iliyowasilishwa kwa Tume ya Maadili na Kukabili Ufisadi, EACC ikimtuhumu Kiunjuri kwa kudai hongo ya shilingi milioni 20.
Katika hati-kiapo hiyo iliyosainiwa na mwanamke kwa jina Delphine Christopher, Kiunjuri kupitia msaidizi wake, Wambui Kimathi alipokea shilingi milioni 10 tarehe 2 mwezi Septemba huku shilingi milioni 10 zaidi zikitarajiwa kulipwa baadaye.
Kiunjuri vile vile alimwachisha kazi kwa muda Mkurugenzi Mkuu wa bodi hiyo, Fazul Mohammed akisema hana tajriba ya kuhudumu katika wadhfa huo.  

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Bold Reporting Takes Time, Courage and Investment. Stand With Us.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902

Follow The Standard on Google News