Hatimaye Kinisu ajiuzulu

Na, Beatrice Maganga

Baada ya shinikizo dhidi yake, hatimaye Mwenyekiti wa Tume ya Maadili na Kukabili Ufisadi, EACC Philip Kinisu amejiuzulu.Kwenye taarifa kwa vyombo vya habari, Kinisu anasema amemwandikia barua Rais kuhusu hatua yake ya kujiuzulu.

Hata hivyo amesisitiza kwamba licha ya kuondoka, kampuni yake ya Esaki Limited haina hatia yoyote kufuatia madai yaliyoibuliwa kwamba ilinufaika kupitia fedha zilizofunjwa kupitia miradi ya Taasisi ya Taifa ya Huduma za Vijana, NYS.

Kinisu amejiuzulu wadhifa huo siku moja baada ya Kamati ya Haki na Sheria iliyo chini ya uwenyekiti wa Mbunge wa Ainabkoi, Samuel Chepkonga kuwasilisha bungeni ripoti ya kupendekeza kuondolewa kwake.Kamati hiyo ilisema sababu zilizowasilishwa dhidi yake zina uzito na iwapo bunge litaidhinisha ripoti hiyo, Rais atabuni jopo la kumchunguza.