Security alert

Usalama umeimairishwa vilivyo katika maeneo mengi humu nchini, kufuatia vitisho vya Al-shabaab kutekeleza mashambulizi msimu huu wa Krismasi. Huko Pwani hasa katika maeneo ya kujivinjari na hata kupumzika mwishoni mwa mwaka, vyombo vya usalama vimeweka mikakati ya usalama wa hali ya juu. Wakati huohuo,bado zile idara za usalama zinatafakari pendekezo la kufutilia mbali tamasha zote za krismasi ili kupunguza uwezekano wa Al-shabaab kulenga maeneo ya mikusanyiko mikubwa ya watu. Itakumbukwa hapo jana waziri wa ulinzi yusuf haji na naibu spika wa bunge Farah Maalim walithibitisha kuwa serikali imechukua hatua za ziada kuwapa ulinzi baada ya kuibuka kuwa Al-shabaab inawalenga kuwaua.

Related Topics

Security alert