Muslim scholars on drugs - Swahili

Serikali imelaumiwa kwa kuzembea katika vita dhidi ya ulanguzi wa dawa za kulevya. Hayo yamesemwa kwenye kongamano la kimataifa linaloendelea huko mombasa la kutafuta mbinu za kupambana na biashara ya mihadarati. Katika kongamano hilo, imependekezwa kwamba sasa kuna haja ya kuzifanyia uchunguzi wa kina meli zinazotia na kungoa nanga katika bandari ya Mombasa.