Mauaji Turkana

Hatimaye maafisa wa polisi wamefika katika kijiji cha Todonyang’ na kukusanya miili ya takriban Waturkana 37 waliouawa jana na wapiganaji kutoka Ethiopia. Aibu kubw kwa serikali ni kwamba watu hao waliuawa kilomita kadhaa ndani ya kenya wala si nchini Ethiopia jinsi ilivyodaiwa jana. John Juma anaangazia baadhi ya maswala mengine ambayo yamedaiwa kuchangia mauaji hayo ambayo waturkana wameamua kuyaita “Todonyang’ Massacre”.