Mbunge wa Keses, Swarup Mishra amesisitiza kwamba atazisaidia familia mia moja za watu wanaofurushwa katika Msitu wa Mau.
Akiwahutubia wanahabari kwenye Eneo Bunge lake, Mishra amesema tayari ametenga ekari kumi na mbili za shamba lake kwa manufaa ya familia hizo mia moja.