×
App Icon
The Standard e-Paper
Fearless, Trusted News
★★★★ - on Play Store
Download App

Ruto asisitiza vita dhidi ya ufisadi vinawalenga baadhi ya watu

Naibu wa Rais William Ruto ameendeleza shtuma dhidi ya baadhi ya watu anaodai kuwa wanatumia vita dhidi ya ufisadi kuisambaratisha miradi ya serikali ya Jubilee. Akizungumza kwenye kaunti ya Mandera wakati alipoongoza shughuli ya utoaji wa chakula cha msaada, Ruto amesema kuwa kwa miaka michache ambayo Jubilee imekuwa madarakani imezipiku zile zilizotanguliwa kupitia rekodi ya maendeleo. Amewataka wanaoishtumu mara kwa mara kukoma kwani wanachochea wananchi wasio na ufahamu wowote kuhusu nia yao potovu.
 
Akionekana kumlenga Kiongozi wa Chama cha ODM Raila Odinga, Ruto amedai kuwa anaendesha siasa za ukabila huku akijidai kuwa anawaunganisha Wakenya.
 
Amesisitiza watakaoamua ni nani kiongozi wa taifa hili, ni Wakenya kupitia uchaguzi mkuu wa mwaka 2022.
 
Hayo yakijiri wabunge wa Chama cha Jubilee wakiongozwa na Kiongozi wa Wengi katika bunge la Kitaifa Adan Duale wametoa wito kwa Rais Uhuru Kenyatta na Naibu wake William Ruto kukilinda chama, wakidai kuna maadui wanaotaka kukisambaratisha.
 
 
 
Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Uncover the stories others won't tell. Subscribe now for exclusive access.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902

Related Topics

ruto Ufisadi