Na Beatrice Maganga
Hatimaye Serikali, Chama cha Wauguzi, KNUN na Baraza la Magavana zimetia saini makubaliano kuhusu matakwa ya wauguzi. Makubaliano hayo yameafikiwa baada ya mapema leo wauguzi kuondoka katika mkutano wa kutafuta mwafaka.
Hata hivyo walirejea katika mkutano huo saa za adhuhuri. Akizungumza wakati wa mkutano wa kutia saini makubaliano hayo, Waziri wa Afya Cleopa Mailu ametoa changamoto kwa madaktari kufuata mkondo huo wa wauguzi na kushiriki mazungumzo ili kupata suluhu.
Mwenyekiti wa Baraza la Magavana Peter Munya vilevile amewataka madaktari kurudi kazini kufuatia agizo lililotolewa jana na Mahakama ya Uajiri na Leba kuwataka wasitishe mgomo.