ELIMU PODCAST; Mzigo wa karo na vitabu; wazazi wanalia
Published Jul. 31, 2021
00:00
00:00

Wazazi nchini Kenya wamepaza sauti kulalamikia hatua ya Wizara ya Elimu kuwapa muda mfupi mno kujitayarisha ili kuwarejesha wanafunzi shuleni kwa muhula wa kwanza ulioanza tarehe 26, Julai, 2021. Wanafunzi takribani 15,000 wamerejea shuleni baada ya likizo ya wiki moja tu suala ambalo limewafanya wazazi kutatizika kutafuta karo na fedha za kununulia vifaa vingine kama vile vitabu. Baadhi ya wazazi walio na watoto zaidi ya mmoja, wamewarai walimu kutowarejesha wanao nyumbani kwa kutokamilisha karo wakiomba kupewa muda zaidi kujiandaa. Wengine nao wanalalamikia hatua ya baadhi ya walimu wakuu kuongeza karo kinyume na mwongozo wa Wizara ya Elimu. Aidha, wameshangaa kupokezwa orodha ndefu ya vitabu vya kusoma kuvinunua ilihali Wizara ya Elimu ilisema imevisambaza katika taasisi za elimu. Mwanahabari wetu Martin Ndiema wa Trans Nzoia amefanya mahojiano nao.