HOJA ZA WAHARIRI PODCAST; Kivumbi kati ya Jubilee na UDA Kiambaa na Muguga
Published Jul. 20, 2021
00:00
00:00

Baada ya chama kipya cha UDA kushinda uchaguzi mdogo wa ubunge kwenye eneo la Kiambaa, kisha Jubilee kukishinda kiti cha uwakilishi wadi Muguga, kivumbi kinatifuka; UDA inaelekea mahakamani kutaka kura za Muguga zihesabiwe upya huku nayo Jubilee ikitaka kura za Kiambaa zihesabiwe tena. Aidha, nani ana ufuasi mkubwa Mlima Kenya baina ya Uhuru Kenyatta na William Ruto? Kuelekea 2022, farasi watakuwa wawili au watatu? Wahariri, Geoffrey Mung'ou na Odeo Sirari wanamshirikisha mwanahabari Victor Mulama aliyekuwa mashinani kuangazia chaguzi hizo, katika kujadili kwa kina masuala haya.