Uzalishaji wa mayai | Uchumi na Biashara Podcast
Published Oct. 24, 2022
00:00
00:00

Licha ya Shirika la Afya Dunia, WHO kushauri kuwa binadamu anafaa kula mayai 180 kwa mwaka, imebainika kwamba taifa la Kenya halijaafikia kiasi hicho takwimu zikionesha kuwa mayai 36 tu huliwa kwa wastani kulinganishwa na mataifa mengine mfano taifa jirani la Uganda na Afrika Mashariki. Hali hii imesababishwa na Wakenya kuzalisha mayai kwa wingi kwa minajili ya kufanya biashara ikilinganishwa na Uganda ambapo huzalishwa vijijini. Mwanahabari wetu Martin Ndiema amesema na wafanyabiashara wa mayai kubaini jinsi uzalishaji na ulaji huathiri biashara yao.