Uchumi na Biashara Podcast; Kilio cha wanabodaboda kwa Rais Kenyatta
Published Mar. 12, 2022
00:00
00:00

Wahudumu wa bodaboda wamewalaumu polisi kwa kuwahangaisha wakitekeleza agizo la Rais kunadhifisha sekta hiyo. Kulingana Wycliffe Nyanamba, Mwenyekiti wa Wanabodaboda hapa jijini Nairobi, polisi wanawahangaisha hadi kwenye makazi yao wakiendesha msako huo wengine wakiwapunja pesa. Hata hivyo, Nyanamba amewalaumu baadhi ya wahudumu hao kwa kukiuka sheria za trafiki. Msako huu unafuatia kisa ambapo wanabodaboda wa Forest Road walimvamia na kumdhulumu kimapenzi mwanamke mmoja. Kauli yake inajiri wakati ambapo oparesheni hiyo imesitishwa kwa muda kupisha mazungumzo.