Mwanaharakati Bob Njagi amedai kuwa kutekwa nyara kwake pamoja na mwenzake Nicholas Oyoo nchini Uganda kulipangwa na serikali ya Kenya. Njagi ameeleza kwamba walikamatwa na kikosi cha kijeshi kinachofanya kazi chini ya uongozi wa Jenerali Muhoozi Kainerugaba wa Jeshi la Ulinzi la Uganda UPDF, huku akiongeza kuwa zaidi ya watu 150 wanazuiliwa bila kufikishwa mahakamani kwa sababu za kisiasa.
Akiwahutubia wanahabari, Njagi alisema kuna ushirikiano kati ya Kenya, Tanzania na Uganda katika kuwakandamiza wakosoaji wa tawala zao, jambo ambalo limeongeza hofu miongoni mwa wanaharakati na viongozi wa upinzani.