Mahakama ya Upeo umeondoa mamlaka ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi IEBC ya kuthibitisha, kujumlisha na kumtangaza mshindi wa uchaguzi wa Urais.
Katika uamuzi wao, Majaji hao saba wakiongozwa na Jaji Mkuu Martha Koome, Naibu wake Philomena Mwilu, majaji Mohammed Ibrahim, Smokin Wanjala, Njoki Ndung'u, Isaac Lenaola vilevile William Ouko wamefafanua kwamba jukumu hilo ni la makamishna wote saba wa IEBC na wala si la mwenyekiti pekee.