Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Fearless, Trusted News
★★★★ - on Play Store
Download App

Vijana wengi walengwa na vyombo vya sheria


Na, Rosa Agutu
Vijana wengi nchini pamoja na raia wenye mapato ya chini wamekuwa wakikandamizwa kisheria pindi wanapotuhumiwa kwa makosa mbalimbali. Hayo yamebainishwa katika ripoti iliyoandaliwa na Baraza la Kitaifa kuhusu Haki na kuzinduliwa rasmi na Jaji Mkuu, David Maraga.  Kulingana na ripoti hiyo, asilimia  75 ya wanaozuliwa kwenye korokoro za polisi ni  vijana wenye kati ya umri wa miaka 18-35. Imebainika kwamba vijana wengi hutiwa mbaroni wakiwa katika harakati za kuendeleza uchuuzi wa kujifatutia riziki bila leseni.
Wengine pia hukamatwa wakiwa katika maeneo ya burudani. Kulingana na Maraga, huo umebainisha kuwa asilimia 63 ya washukiwa wa makosa mblimbali huachiliwa huru bila kuwepo kwa rekodi rasmi kuhusu sababu za kuachiliwa kwao.
Aidha, ripoti hiyo inaonyesha kwamba asilimia 49 ya visa vya mauaji vimetekelezwa na wanawake ikilinganishwa na asilimia 32 ya wanaume. Vilevile kesi nyingi za wizi wa bidhaa zimewahusishwa wanawake walioajiriwa kuwa vijakazi wa nyumbani.
Licha ya ripoti hiyo kubainisha kwamba visa vya unajisi wa watoto vimeongezeka, ni asilimia tano pekee ya visa hivyo ambapo wahusika huhukumiwa huku asilimia 60 ya kesi hizo zikiondlewa mahakamani.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mwanasheria Mkuu wa serikali, Prof Githu Muigai amesema ripoti hiyo itasaidia kukabili visa vya ubaguzi na kuhakikisha wananchi wanatendewa haki. Na huku shughuli ya kuwasajili wapigakura wapya ikiendelea, Muigai ametoa wito kwa Tume ya Uchaguzi, IEBC kufanikisha usajili wa wafungwa.  

 

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Fact-first reporting that puts you at the heart of the newsroom. Subscribe for full access.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902

Follow The Standard on Google News

Related Topics