Na, Sophia Chinyezi
Tofauti zinaendelea kuibuka kuhusiana na hoja zilizowasilishwa na mwanaharakati mmoja kuhusu kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Tume ya Maadili na Kukabili Ufisadi EACC, Phillip Kinisu. Kinisu anachunguzwa kufuatia madai kwamba kampuni yake ya Esaki ililipwa zaidi ya shilingi milioni thelathini na tano kupeleka vifaa vya kuchimba kisima katika Taasisi ya Taifa ya Huduma za Vijana NYS, kati ya mwezi Oktoba 2014 na Novemba 2015.