×
App Icon
The Standard e-Paper
Stay Informed, Even Offline
★★★★ - on Play Store
Read on the App

Rais akwepa kulizungumzia suala la mishahara ya polisi.

Kinyume na ilivyotarajiwa, Rais Uhuru Kenyatta amekwepa kuzungumzia suala lililochochea hisia kali la maafisa wa polisi kupungiziwa mishahara, badala yake kulenga masuala mengine yanayohusu usalama wa nchi. Akizungumza alipoongoza hafla ya kufuzu kwa makurutu katika Chuo cha Mafunzo cha Kiganjo, Rais amesema mpango wa kushirikiana miongoni mwa taasisi mbalimbali wakati wa kukabili visa vya utovu wa usalama nchini, umechangia pakubwa kukabiliwa kwa tishio hilo. Amezitaja hatua zilizopigwa kuwakabili magaidi kuwa mojawapo ya mafanikio hayo. Rais amesema ana imani kuwa waliofuzu leo wataendeleza mpango huo wa serikali.

Rais aidha amewashauri kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na kuzingatia waliofunzwa chuoni humo katika utendakazi wao. Rais amewashauri kudumisha uhusiano mwema na raia wa maeneo watakayotumwa kuhudumu ili kuboresha sifa za idara hiyo.

Get Full Access for Ksh299/Week
Uncover the stories others won’t tell. Subscribe now for exclusive access
  • Unlimited access to all premium content
  • Uninterrupted ad-free browsing experience
  • Mobile-optimized reading experience
  • Weekly Newsletters
  • MPesa, Airtel Money and Cards accepted
Already a subscriber? Log in

Related Topics